BEKI LA NGUVU KAZE GILBERT NA MSHAMBULIAJI HATARI TAMBWE WAREJEA KAZINI SIMBA SC
BEKI Kaze Gilbert aliyeumia nyonga Jumamosi Simba SC
ikimenyana na Mbeya City na kutoka sare ya 2-2 katika Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara, anatarajiwa kurejea mazozini leo baada ya kupona.
Aidha, Mrundi mwenzake Amisi Tambwe aliyeumia pia nyama
katika mchezo huo uliokuwa mkali na wa kusisimua, naye anatarajiwa kuanza
mazoezi leo.
Daktari wa Simba SC, Yassin Gembe ameiambia BIN ZUBEIRY leo
kwamba, mbali na Warundi hao wawili waliosajiliwa kutoka Vital’O ya Burundi,
majeruhi mwingine ni kiungo Henry Joseph ambaye anasumbuliwa na maumivu ya
goti.
Warundi wawili; Kaze Gilbert na Amisi Tambwe wote wanarejea
mazoezini leo
“Henry bado kidogo, nadhani kuanzia kesho tunaweza kujua
anaweza kuanza lini mazoezi. Lakini Kaze na Tambwe wote tunawatarajia leo
wataanza mazoezi,”alisema.













.jpg)








0 comments:
Post a Comment