BEKI LA NGUVU KAZE GILBERT NA MSHAMBULIAJI HATARI TAMBWE WAREJEA KAZINI SIMBA SC

BEKI Kaze Gilbert aliyeumia nyonga Jumamosi Simba SC ikimenyana na Mbeya City na kutoka sare ya 2-2 katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, anatarajiwa kurejea mazozini leo baada ya kupona.
Aidha, Mrundi mwenzake Amisi Tambwe aliyeumia pia nyama katika mchezo huo uliokuwa mkali na wa kusisimua, naye anatarajiwa kuanza mazoezi leo.
Daktari wa Simba SC, Yassin Gembe ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba, mbali na Warundi hao wawili waliosajiliwa kutoka Vital’O ya Burundi, majeruhi mwingine ni kiungo Henry Joseph ambaye anasumbuliwa na maumivu ya goti.

Warundi wawili; Kaze Gilbert na Amisi Tambwe wote wanarejea mazoezini leo


“Henry bado kidogo, nadhani kuanzia kesho tunaweza kujua anaweza kuanza lini mazoezi. Lakini Kaze na Tambwe wote tunawatarajia leo wataanza mazoezi,”alisema.

0 comments:

Post a Comment