TANGU kustaafu kwa Lennox Lewis hajatokea mbabe mwingine mwenye mvuto katika ndondi za uzito wa juu, lakini Jumamosi usiku Anthony Joshua alionyesha anaweza kurudisha raha katika masumbwi ya uzito wa juu. Mbabe huyo wa London na mshindi wa Medali ya Dhahabu ya Olimpiki, alianza vyema ndondi za kulipwa kwa kumpiga mpinzani wake Emanuele Leo kwa Knockou (KO) Raundi ya kwanza ukumbi wa O2 Arena. Chali, kwisha kazi : Anthony Joshua (kushoto) akiwa amemdondosha Emanuele Leo katika Raundi ya kwanza kwenye pambano lake la kwanza la ndondi za kulipwa Tayari anatabiriwa kuwa Lennox Lewis mwingine na kutamba katika ulimwengu wa ndondi hadi kuwa bingwa asiyepingika wa uzito wa juu duniani.

Kazi nyepesi: Joshua alianza vyema maisha ya ndondi za kulipwa

Ana ngumi nzito Anatisha kijana: Joshua atarejea ulingoni baadaye mwezi huu ili kujijenga zaidi Mwisho, konde la nguvu la Joshua limetua kichwani kwa jamaa
BEKI Kaze Gilbert aliyeumia nyonga Jumamosi Simba SC ikimenyana na Mbeya City na kutoka sare ya 2-2 katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, anatarajiwa kurejea mazozini leo baada ya kupona.
Aidha, Mrundi mwenzake Amisi Tambwe aliyeumia pia nyama katika mchezo huo uliokuwa mkali na wa kusisimua, naye anatarajiwa kuanza mazoezi leo.
Daktari wa Simba SC, Yassin Gembe ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba, mbali na Warundi hao wawili waliosajiliwa kutoka Vital’O ya Burundi, majeruhi mwingine ni kiungo Henry Joseph ambaye anasumbuliwa na maumivu ya goti.

Warundi wawili; Kaze Gilbert na Amisi Tambwe wote wanarejea mazoezini leo


“Henry bado kidogo, nadhani kuanzia kesho tunaweza kujua anaweza kuanza lini mazoezi. Lakini Kaze na Tambwe wote tunawatarajia leo wataanza mazoezi,”alisema.
MWENYEKITI wa Yanga SC, Alhaj Yussuf Mehboob Manji amewaambia wachezaji wa timu hiyo kwamba hana matatizo nao kwa matokeo ya awali ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na amewataka waelekeze nguvu zao katika mechi zijazo.
Yanga imeambulia pointi sita katika mechi tano za awali za Ligi Kuu ya Vodacom, kutokana na sare tatu, kushinda moja na kufungwa moja, hivyo kuachwa kwa pointi tano kileleni na wapinzani wao wa jadi, Simba SC.
Jana Manji alikutana kwa chakula cha jioni na wachezaji wa timu hiyo katika hoteli ya Serena, Dar es Salaam akiwa ameambatana na Makamu wake Mwenyekiti, Clement Sanga, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Isaac Chanji na Mjumbe wa Sekretarieti, Patrick Naggi.


Manji akipeana mkono na Chuji alipokutana na wachezaji hao mwaka jana.

Katika kikao hicho, Manji aliwaambia wachezaji wa Yanga hamlaumu yeyote kwa matokeo hayo, kwani ligi bado mbichi, ila akawataka waunganishe nguvu zao kuelekea mechi zijazo, ili kurejesha ushindi na furaha klabuni.
Pamoja na hilo, Manji alizungumzia suala la madai ya baadhi ya wachezaji ya fedha za usajili na akaliweka sawa kwa wale ambao walikuwa wanadai kuwawekea utaratibu wa malipo haraka, jambo ambalo Naggi ametakiwa kuhakikisha analishughulikia mara moja.
Aidha, Manji baada ya kikao cha pamoja na wachezaji wote, alimvuta pembeni Mrisho Ngassa kujadiliana naye faragha.

Haikujulikana mara moja Manji alizungumza nini na Ngassa, lakini inaweza kuwa kuhusu deni analotakiwa kuilipa Simba SC, Sh. Milioni 45 kwa kosa la kusaini Mikataba na timu mbili. Ngassa alifungiwa mechi sita za mashindano na kutakiwa kurejesha fedha alizochukua Simba SC Sh. Milioni 30 pamoja na fidia ya Sh Milioni 15.

MRISHO Khalfan Ngassa amepata timu ya Oman inayotaka kumnunua kutoka Yanga SC pamoja na kulipa deni la Simba SC, Sh. Milioni 45, lakini uongozi wa klabu yake kama unamuwekea kauzibe hivi.
Habari za ndani ambazo BIN ZUBEIRY imezipata juu ya sakata la Ngassa na Yanga ni kwamba, mchezaji huyo amepata timu inayotaka kumnunua moja kwa moja, ikiwa tayari kutoa kiasi cha Sh. Milioni 100, ambazo zitalipa deni la Simba na nyingine kulipwa Yanga ambao wana Mkataba naye kwa sasa.
Hata hivyo, wakati Yanga ikimzuia Ngassa kwenda Oman, nayo inaonekana kusuasua kumilipia deni la Simba SC.
Habari zinasema Yanga wametaka kumsainisha Ngassa Mkataba wa kumlipia deni, lakini amegoma kuusaini kwa kuhofia kurudia kosa alilofanya kusaini Mkataba na Simba SC ambao hakuuelewa.

Mpenzi wa Yanga; Mrisho Ngassa amegoma kusaini kichwakichwa fomu za kulipiwa deni

“Ngassa ameshituka sasa hivi, amegoma kusaini huo Mkataba wa kulipiwa deni, kwanza hadi aupeleke kwa Wakili wake akaupitie. Unajua Simba walimuambia anasaini kukubali kucheza kwa mkopo, kumbe anasaini Mkataba mpya, sasa amekuwa mjanja sana sasa hivi,”kilisema chanzo.
Chanzo hicho kimesema kwamba, Yanga inataka kumlipia Ngassa deni na kuongeza miaka miwili katika Mkataba wake kutoka miwili ya sasa, lakini yeye mwenyewe mchezaji amependekeza alipiwe deni hilo na baada ya hapo atakuwa anakatwa kwenye mshahara wake.
Hadi sasa Ngassa hajasaini hati aliyotakiwa kusaini alipiwe deni hilo, maana yake kuna hatari akashindwa kuanza kucheza Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Jumamosi dhidi ya Ruvu Shooting, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Ikumbukwe Ngassa alifungiwa mechi sita za mashindano kwa kosa la kusaini Mikataba na timu mbili, Simba na Yanga SC. Pamoja na adhabu hiyo aliyomalizia Jumapili, Ngassa alitakiwa kurejesha fedha alizochukua Simba SC Sh. Milioni 30 pamoja na fidia ya Sh Milioni 15, jumla Milioni 45.
MAMLAKA za Mkoa wa Mwanza zimesema zitatimiza ahadi yao ya kuchangia dola 118,000 za Marekani (zaidi ya sh. milioni 190) ili kukamilisha mradi wa kuweka nyasi bandia kwenye Uwanja wa Nyamagana, jijini Mwanza kabla ya Oktoba 15 mwaka huu.
Mkuu wa Mkoa (RC) wa Mwanza, Mhandisi Evarist Ndikilo pamoja na Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza, Stanslaus Mabula wametoa ahadi hiyo wakati wa kikao kati yao na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga kilichofanyika leo (Septemba 25 mwaka huu) kwenye ofisi za TFF.


Rais wa TFF, Leodegar Tenga (wa pili kushoto) akiwa na ujumbe wa Mkoa wa Mwanza ulioongozwa na Mkuu wa Mkoa, Mhandisi Evarist Ndikilo ulipomtembelea katika ofisi za TFF jana. Wa tatu kutoka kushoto ni Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza, Stanslaus Mabula akifuatiwa na Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Hida Hassan.

Wakuu hao wa Mwanza katika kikao hicho pia walifuatana na Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Hida Hassan.
TFF ilipeleka mradi wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) wa Goal Project IV wa nyasi bandia wa dola 500,000 za Marekani katika Uwanja wa Nyamagana.
Mradi huo ulipelekwa huko baada ya Mkoa wa Mwanza kuahidi kuchangia dola 118,000 ili kukamilisha thamani ya mradi mzima ambayo ni dola 618,000 za Marekani. Wamiliki wa uwanja huo ni Jiji la Mwanza.

Goal Project I ilitumika kwa ajili ya ujenzi wa hosteli ya TFF (technical centre), Goal Project II nyasi bandia Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume wakati Goal Project III iliweka nyasi bandia katika Uwanja wa Gombani ulioko Pemba, Zanzibar.
RHINO Rangers imepata ushindi wa kwanza katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu huu, baada ya leo kuilaza Ashanti United mabao 2-0 Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi, Tabora.
Kwa ushindi huo, timu hiyo ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) imefikisha pointi saba na kupanda hadi nafasi ya nane ikiwashusha kwa nafasi moja, mabingwa watetezi, Yanga SC.


Juu ya mabingwa; Rhino leo wameishusha Yanga kwa nafasi moja

Katika mchezo huo, mabao ya Rhino yalifungwa na Kamana Salum dakika ya 26 na Hussein Abdallah dakika ya 64.
Ligi hiyo itaendelea Jumamosi wakati, Yanga SC itakapomenyana na Ruvu Shootings Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na Rhino Rangers wakiikaribisha Ashanti United Mwinyi, Tabora.

Mechi nyingine zitapigwa Jumapili, Simba SC ikishuka dimbani Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kumenyana na JKT Ruvu, Rhino Rangers na Kagera Sugar Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi, Tabora, Mbeya City na Coastal Union Sokoine, Mbeya, Mgambo JKT na JKT Oljoro Mkwakwani, Tanga na Ashanti United na Mtibwa Sugar, Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
MACHO yote yalikuwa kwa Luis Suarez baada ya kurejea Liverpool kufuatia kumaliza adhabu yake ya mechi 10, lakini Javier Hernandez akaiteka shoo kwa bao lake pekee lililoipeleka Manchester United Raundi ya Nne ya Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One.
Hatimaye Suarez alicheza mechi yake ya kwanza ya msimu mpya baada ya kumaliza kutumikia adhabu yake ya kumng'ata beki wa Chelsea, Branislav Ivanovic msimu uliopita.
Na wakati mshambuliaji huyo wa Uruguay alizomewa na mashabiki Uwanja wa Old Trafford, alikuwa ni Chicharito aliyepoza maumivu ya David Moyes kufuatia kipigo cha mabao 4-1 kutoka kwa wapinzani, Manchester City katika Ligi Kuu Jumapili.
Liverpool ilitawa sehemu kubwa ya mchezo na Daniel Sturridge alipoteza nafasi kadhaa nzu za kufunga, lakini Hernandez hakufanya makosa alipopata nafasi dakika ya 46.
Wayne Rooney, ambaye ndiye mchezaji bora zaidi kwa United hivi sasa, alipiga kona nzuri baada ya mapumziko na Hernandez akaunganisha nyavuni.
Kikosi cha Manchester United kilikuwa: De Gea, Rafael Da Silva, Smalling, Evans, Buttner, Jones, Giggs, Nani, Rooney, Kagawa na Hernandez.
Liverpool: Mignolet, Toure, Skrtel, Sakho, Jose Enrique, Gerrard, Lucas, Henderson, Suarez na Moses, Sturridge. 


Shujaa: Javier Hernandez akishangilia baada ya kufunga bao pekee la Manchester United Uwanja wa Old Trafford
KLABU ya Arsenal itamenyana na wapinzani wao katika Jiji la London, Chelsea katika Raundi ya Nne ya Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One Cup baada ya kuitoa West Brom kwa penalti 4-3 Uwanja wa Hawthorns.
Mechi hiyo imeisha kwa sare ya 1-1 usiku huu, lakini penalti walizokosa Morgan Amalfitano na Craig Dawson zinawasongesha mbele Gunners.


Mbele: United imesonga mbele kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya Liverpool Uwanja wa Old Trafford

RATIBA KAMILI RAUNDI YA NNE CAPITAL ONE
Sunderland v Southampton
Leicester City v Fulham
Birmingham City v Stoke City
Manchester United v Norwich City
Burnley v West Ham United
Arsenal v Chelsea
Tottenham v Hull City
Newcastle v Manchester City
Mechi zote zitachezwa Jumanne ya Oktoba 29 na Jumatano ya Oktoba 30.
Manchester United baada ya kuwatoa wapinzan wao, Liverpool watamenyana na Norwich nyumbani katika Raundi ya Nne.
Bao pekee la Javier Hernandez mapema kipindi cha pili katika ushindi wa 1-0 Old Trafford, linawakutanisha Mashetani Wekundu na The Canaries Oktoba 28.
Birmingham iliyowatoa mabingwa watetezi Swansea kwa mabao 3-1 watacheza tena nyumbani katika 16 Bora, safari hii wakimenyana na timu ya Mark Hughes, Stoke.
Licha ya kupangiwa wapinzani wagumu, lakini The Blues bado wanapewa nafasi kubwa ya kutwaa tena taji walilolitwaa mwaka 2011, na United ikiwa timu nyingine inayopewa nafasi pia baada ya kupangiwa Norwich.
Katika mechi nyingine, Newcastle itaikaribisha Manchester City Uwanja wa St James Park baada ya kuwatoa Leeds, wakati Hull wataifuata Tottenham siku kadhaa baada ya kucheza mechi ya Ligi Kuu, Uwanja wa White Hart Lane.
Timu isiyo na kocha kwa sasa, Sunderland itamenyana na Southampton, wakati West Ham watakwedna Kaskazini kumenyana na Burnley.
Fulham ya Martin Jol itaifuata Leicester kusaka nafasi ya Robo Fainali.
MIKWAJU YA PENALTI
West Brom: Reid (penalti ya kwanza) amefunga, Rosenberg amefunga, Morrison amefunga, Dawson amekosa, Amalfitano amekosa
Arsenal: Bendtner amefunga, Gnabry amekosa, Olsson amefunga, Akpom amefunga, Monreal amefunga
Arsenal imeifunga West Brom kwa penalti 4-3
Arsenal iliendeleza wimbi la ushindi kwa kuitoa kwa matuta West Brom Uwanja wa The Hawthorns na kuingia Raundi ya Nne.
Eisfeld aliifungia Arsenal dakika ya 61 kabla ya Berahino kusawazisha dakika ya 71.
Kikosi cha West Brom kilikuwa: Daniels, Reid, Popov, Lugano, Dawson, Sinclair, Dorrans, Mulumbu/Morrison dk91, Berahino/Amalfitano dk101, Long/Rosenberg dk91, Sessegnon
Arsenal: Fabianski, Mertesacker, Vermaelen, Monreal, Jenkinson, Arteta/Bellerin dk95, Miyaichi, Gnabry, Hayden/Kris Olsson dk84, Bendtner, Eisfeld/Akpom dk82.



Ya ushindi: Nacho Monreal akiifungia Arsenal penalti ya ushindi
PAMOJA na kumkosa mchezaji ghali duniani, Gareth Bale, lakini mchezaji anayeliwa mshahara mkubwa zaidi duniani, Cristiano Ronaldo alitosha kuipa pointi tatu Real Madrid usiku huu, baada ya kufunga mabao yote katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Elche.
Bale atarejea katika mechi ya nyumbani na Atletico Madrid Jumamosi wakati leo Ronaldo, ameendelea kuiweka Real karibu vinara wa La Liga.
Ronaldo alifunga mabnao hayo katika dakika za 51 na dakika ya sita ya muda wa nyongeza baada ya kutimu dakika 90, wakati bao la kufutia machozi la Elche lilifungwa na Richmond Boakye dakika ya pili ya muda wa nyongeza baada ya kutimua dakika 90.
Kikosi cha Elche kilikuwa: Elche: Manu Herrera; Damián, Botía, Lombán, Albácar; Rubén Pérez, Carlos Sánchez; Stevanovic, Coro, Fidel na Boakye.
Real Madrid: Diego López, Pepe, Ramos, Coentrão, Khedira, Ronaldo, Benzema, Arbeloa, Modric, Di María na Isco.


Raha: Ronaldo akishangilia baada ya kuifungia Madrid bao la pili


Moja zaidi: Cristiano Ronaldo akishangilia na wachezaji wenzake


Weka kule: Real Madrid ilicheza bila mchezaji ghali duniani, Gareth Bale



Beki wa Elche, Botia (kushoto) akikabiliana na mshambuliaji Mfaransa wa Real Madrid, Karim Benzema
TOUT Puissant Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), itaanzia ugenini Nusu Fainali ya kwanza ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Stade Malien ya Mali, Oktoba 6, mwaka huu, kabla ya kurudiana wiki mbili baadaye mjini Lubumbashi.
Kwa mujibu wa Ratiba iliyotolewa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) jana, mchezo wa kwanza utachezwa kwenye Uwanja wa Modibo Keita mjini Bamako kuanzia saa 10:00 jioni kwa saa za huko na saa 12:00 kwa saa za Afrika Mashariki.


Mapacha watatu; Kutoka kulia Thomas Ulimwengu, Tresor Mputu na Mbwana Samatta washambuliaji hatari wa Mazembe ambao wanafunga karibu kila mechi

Mechi hiyo itachezeshwa na refa Alioum Neant, atakayesaidiwa na Evarist Menkouande wote wa Cameroon na Peter Edibi wa Nigeria, wakati refa wa akiba atakuwa Mohamadou Mal Souley pia wa Cameroon.
Timu hizo zitarudiana Oktoba 19, Uwanja wa Mazembe mjini Lubumbashi, zikichezeshwa na marefa Haimoudi Djamel wa Algeria atakayesaidiwa na Achik Redouane wa Morocco na Etchiali Abdelhak wa Algeria, wakati refa wa akiba atakuwa Bousseter Sofiane  wa Algeria pia.
Mazembe inayoongozwa na washambuliaji wawili wa Kitanzania, Mbwana Ally Samatta na Thomas Emmanuel Ulimwengu, ikifanikiwa kuitoa Stade Malien itamenyana na mshindi wa Nusu nyingine, kati ya timu za Tunisia tupu, Club Africaine na C.S. Sfaxien.

Ikumbukwe Mazembe iliangukia kwenye Kombe la Shirikisho baada ya kutolewa na Orlando Pirates ya Afrika Kusini katika 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu na sasa inaelekea kufuta machungu kwa kutwaa taji hilo la pili kwa ukubwa kwa michuano ya klabu Afrika.